
( Mjadala juu ya digrii ya Adam Malima uliibuka na kujadiliwa kwa kina mwanzoni mwa mwaka huu. Leo hii, tukiwa tukaribia mwisho wa mwaka, Bw. Nalitolela amekuja na hoja. Kwanza tutakumbushua hoja iliyoibua mjadala hapo chini na kisha tutaona ufafanuzi wa Nalitolela.
"Jamani hizi digrii za Adam Malima zinatambuliwa na Taasisi ya Elimu ya juu Tanzania?
Kufuatana na tovuti ya Bunge mheshimiwa Adamu Malima alipomaliza kidato cha nne alienda kusoma Chuo kikuu cha HAVANA CUBA digrii ya pili.Yaani kutoka kidato cha nne hadi kusoma digrii ya pili.Halafu akaenda SOAS alikosomea Postgraduate diploma na Masters degree tena.Je hizo degree zote alizonazo huyo mheshimiwa zina hadhi ya kutambuliwa na mamlaka ya Elimu Tanzania hadi kumwezesha mtu apewe unaibu uwaziri?
Kufuatana na Tovuti ya bunge
http://www.parliament.go.tz/bunge/mp_Cv3.asp?PTerm=2005-2010&fpkey=427
Elimu ya Huyo mheshimiwa ni kama ifuatavyo:
University of London (SOAS) MSc (Econ) 1994 - 1995 MASTERS DEGREE
Univesity of London (SOAS) Post Graduate Diploma (Econ) 1993 - 1994
POSTGRADUATE
University of Havana (Cuba) MSc (Economicy) 1984 -1989 MASTERS DEGREE
Shaban Robert Secondary School O-Level Education 1979 - 1982 SECONDARY
Upanga Primaru School Primary Education 1972 - 1978 PRIMARY
Hizo digrii za Cuba na hizo za SOAS zinatambuliwa hapa Tanzania?"
: Wed Dec 02, 07:26:00 AM EAT, Nalitolela, P. S.
Nilikuwa nikisaka habari fulani katika mtandao nikakutana na picha ya waheshimiwa na kusoma maoni juu hapo. Simtetei Malima wala simpingi, ila naomba niseme yafuatayo:
1. Katika baadhi ya nchi shahada ya uzamili (master's) huwa inaunganishwa na shahada ya kwanza na unasoma kwa miaka mitano, hivyo unapohitimu unapewa MA/MSc moja kwa moja. Cuba ni nchi mojawapo; pia nchi nyingi za Ulaya Mashariki ikiwamo Urusi zilikuwa zina mtindo huu na baadhi wanaendelea nao.
2. Chuo Kikuu cha Havana ni chuo kinachofahamika na kuheshimika kimataifa. Mfano kuna Professor anafundisha Ryerson University, Canada. Tovuti yake nii hapa: http://www.math.ryerson.ca/~polivares/
Huyu jamaa kasoma PhD Havana na kama ingekuwa chuo hiki hakitambuliki huyu bwana asingepata kazi Ryerson (http://www.ryerson.ca/home.html, http://en.wikipedia.org/wiki/Ryerson_University)
3. Suala la kutoka kidato cha 4 kwenda chuo kikuu sio la ajabu. Kuna mtu namfahamu alimaliza kidato cha 4 Tanzania, akaanza cha 5. Katikati ya kidato cha 5 akapata nafasi kusoma Canada katika chuo kikuwa kinachotambulika (University of New Brunswick). Katika baadhi hawana system ya A level; hata kama elimu yao ina miaka 6 ya Sekondari. Hivyo basi kwa mtu uliyehitimu kidato cha 6 Bongo inakuwa kama umesoma 1st year tayari, na unaruhusiwa kuanza masomo ya 2nd year. Hivyo basi kwa mtu aliyehitimu form 5 na kufanya vyema, anaweza kuacha kusoma A level na kuanzia 1st year. Kila nchi ina system tofauti. Cha muhimu sio umesoma kwa miaka mingapi; cha muhimu umesoma "deep" kiasi gani.
4. Ndio maana nchi kam Uingereza waliamua kufanya bachelor zao karibia zote ziwe miaka mitatu, sio kama nyumbani ambapo bado baadhi ya discipline ni miaka minne, nyingine mitatu.
5. Mara kwa mara nimeona mijadala kama hii mtandaoni. Mfano baadhi ya watu nimeshaona wakihoji mtu kutoka "Bachelors" hadi "PhD". Kwenye nchi nyingi, ikiwemo Uingereza, Marekani na Australia, kusoma Master's sio lazima na Master's kwa kawaida ni professional degree. Kwa wale wanaotaka kufanya research wanaenda PhD moja kwa moja.
6. System zipo tofauti, cha muhimu utambulike kimataifa. Mfano baadhi ya nchi Master's karibia zote ni mwaka mmoja; wakati nchi nyingine Master's ni miaka miwili.